Saturday, April 30, 2016

MOURINHO TAYALI KUTUA MAN UNITED

OSE MOURINHO amepewa uhakika katika masaa 48 yaliyopita kwamba atakuwa kocha mpya wa Manchester United.
  Kambi yake ilikuwa na wasiwasi kwamba United walikuwa wanamfikiria Laurent Blanc aje kuungana na Giggs kama ilivyoripotiwa mapema wiki hii. Lakini ameambiwa yeye ndiye anaetakiwa na wafanya maamuzi wa Old Trafford.
  Mazungumzo yameshafikia mwishoni na karibia kumalizika ndani ya siku 10 zijazo. 
Tangu mwezi wa 12 kulikuwepo na taarifa kwamba United wamefanya mawasiliano na Mourinho siku chache baada kocha huyo kufukuzwa Na Chelsea.
Aliambiwa wanamhitaji na asichukue majukumu ya sehemu nyingine. 
Tangu wakati huo United wanaripotiwa kumpa mkataba wa miaka 3 wenye thamani ya £60m ambao utamfanya mreno huyo kuwa kocha atakayelipwa zaidi katika historia. 
United pia walijaribu kuangalia upatikanaji wa  Maurico Pochettino wa Spurs na kocha  Paris Saint-Germain Blanc, wakati baadhi ya watu ndani ya klabu walijaribu kutaka Giggs apandishwe cheo. 
  Lakini Mourinho siku zote anawashinda wapinzani wake katika kazi hiyo mbele yenye wenye maamuzi Old Trafford na hilo limewekwa wazi kabisa na kumuondolea mashaka kabisa Mourinho wiki hii. 
United wanafahamu kwamba Mourinho hawezi kukosa ofa nzuri na hii ni nafasi yao ya mwisho kumpata. 

SOURCE;SHAFFIHDAUDA

No comments:

Post a Comment