
FC Barcelona hawakuwa tayari kuona wakiweka rekodi ya kufungwa kwa mara ya pili mfululizo katika uwanja wao wa nyumbani, licha ya kuwa walianza kufungwa goli dakika ya 25 na Fernando Torres, ila Luis Suarez ndio akaiokoa FC Barcelona kwa kufunga magoli mawili dakika ya 63 na 74 na kuendeleza rekodi ya kufunga jumla ya goli 8 katika mechi 8.
Kazi imebakia kwa klabu ya Atletico Madrid April 13 kuisubiri FC Barcelona katika mchezo wao wa marudiano ambao ndio mchezo utakaoamua nani afuzu kucheza nusu fainali ya michuano ya klabu Bingwa Ulaya msimu wa 2015 /2016. Kwa upande wa FC Bayern wao wameibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Benfica.
SOURCES;MILLARD AYO