Wednesday, April 06, 2016

BAYERN ,BARCA ZASHINDA USHINDI MWEMBAMBA NYUMBANI BADO NGOMA MBICHII..

32E0373C00000578-3525212-image-a-57_1459888396328
FC Barcelona hawakuwa tayari kuona wakiweka rekodi ya kufungwa kwa mara ya pili mfululizo katika uwanja wao wa nyumbani, licha ya kuwa walianza kufungwa goli dakika ya 25 na Fernando Torres, ila Luis Suarez ndio akaiokoa FC Barcelona kwa kufunga magoli mawili dakika ya 63 na 74 na kuendeleza rekodi ya kufunga jumla ya goli 8 katika mechi 8.
Kazi imebakia kwa klabu ya Atletico Madrid April 13 kuisubiri FC Barcelona katika mchezo wao wa marudiano ambao ndio mchezo utakaoamua nani afuzu kucheza nusu fainali ya michuano ya klabu Bingwa Ulaya msimu wa 2015 /2016. Kwa upande wa FC Bayern wao wameibuka na ushindi wa goli 1-0 dhidi ya Benfica.

SOURCES;MILLARD AYO

OFFICIAL YAYA TOURE ANAONDOKA MAN CITY.



Ni kitambo toka tuanze kusoma vichwa vya habari kwenye Magazeti vikisema ….Yaya Toure kuondoka Man City >>> <<< Man City wamuahidi Yaya Toure asiondoke <<< 
Baada ya hivyo vichwa vya habari, taarifa iliyothibitishwa April 4 2016 na wakala wa Yaya inasema hivi >>> ‘Tumesubiri kwa muda mrefu lakini Man City hawajatekeleza chochote kwenye ahadi walizotoa kwahiyo Yaya ataachana na hii club June.

MONEY TALK.....MISHAHALA YA MAKOCHA KWENYE EPL ...



Kocha Antonio Conte amejiunga Chelsea kwa dau la pauni milioni 6.5 lakini Arsene Wenger anachukua pauni milioni 8.5.

Wengine wanaochukua fedha ndefu ni Louis van Gaal anayechukua pauni milioni 7.3 na Pochettino wa Tottenham wa Spurs anachukua pauni milioni 3.5 huku Claudio Ranier ambaye timu yake ya Leicester iliyo kileleni anachukua pauni milioni 1.5.

Kocha wa zamani wa Chelsea, Jose Mourinho alikuwa anachukua pauni milioni 13.2. Lakini  Pep Guardiola ambaye ni kocha mpya wa Manchester City atakuwa anakula mkwanja zaidi kwa kuchukua pauni milioni 15 ambae msimu ujao ankuwa kocha wa man city.

Sources ;salehjembe