Monday, April 04, 2016

ANTONIO CONTE KUWA MRITHI WA MOURINHO CHELSEA.....

Conte-deal done
      Antonio conte kocha wa timu ya Italy kwa sasa ambapo mashindano ya Euro yakiisha anakuwa                                                                kocha wa chelsea.

Leo April 4, klabu ya Chelsea imethibitisha kukubaliana Conte kuwa kocha wao akichukua mikoba ya aluyekuwa kocha wa timu hiyo Jose Mourinho.
Conte amesaini deal la miaka mitatu na The Blues, kisha akatoa maneno yafuatayo kwenye website ya Chelsea:
Nimefurahi sana kupata fursa ya kufanya kazi kwenye klabu ya Chelsea. Najivunia kuwa kocha wa timu ya taifa ya nchi yangu pia kuivutia klabu kama Chelsea na kupewa jukumu la kuifundisha.
Natarajia kukutana na kila mmoja kwenye klabu pamoja na kupambana kila siku na changamoto za michuano ya Premier League.
Chelsea pamoja na soka la Engand linatazamwa popote utakapoenda, lengo langu ni kupata mafanikio zaidi kama yale ambayo nimekuwa nikiyafurahia Italy. 
Nimefurahi tumeshaweka wazi kilakitu kwahiyo kilakitu kiko sawa na tumemaliza tetesi zote. Nitaendelea na kazi yangu kama kocha wa timu ya taifa ya Italy na kwasasa sitazungumza tena kuhusu Chelsea hadi fainali za Euro zitakapomalizika.

No comments:

Post a Comment